Pages

  • Latest News

    Tuesday, 14 April 2015

    FAMILIA YA LOWASSA YAPELELEZWA LONDON.

    MTOTO wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa anayeitwa Frederick Lowassa anachunguzwa na Kitengo Maalumu cha Polisi wa Kimataifa wa Uingereza wanaofuatilia utata wa uhamishaji fedha kutoka Tanzania.
    Fedha hizo zinahusishwa na ununuzi wa nyumba yenye thamani ya paundi za Uingereza 475,000 (takriban Shilingi bilioni moja) katikati ya Jiji la London. Nyumba hiyo ipo mtaa wa Leinster Gardens, jijini London.
    Hata hivyo, hakuna ofisa yeyote wa Serikali ya Tanzania aliyekuwa tayari kuzungumzia suala hilo, pamoja na kuwapo taarifa kwamba tayari vyombo vya dola vya Tanzania vimekwisha kuhusishwa katika uchunguzi huo.
    Maofisa wa Polisi wa Idara ya Upelelezi wa Jinai (CID) wanaohusika na uchunguzi wa fedha haramu, pamoja na Mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa ya jinai (DCI) Robert Manumba, wamekwepa kuzungumzia suala hilo.
    Source: Raia Mwema, Toleo la 161
    HIVI WATANZANIA TUMELOGWA???
    KWA NINI TUNAPENDA KUSHABIKIA MAOVU??

     LOWASSA HAFAI KABISA KUWA HATA BALOZI WA NYUMBA KUMI
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: FAMILIA YA LOWASSA YAPELELEZWA LONDON. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top