Pages

  • Latest News

    Tuesday, 14 April 2015

    Yanga yatumia mil288 kuikomesha Simba

     JUMAMOSI kutakuwa na fleva fulani hivi kwenye kabumbu. Mashabiki wa Manchester United, Chelsea na Arsenal watashuhudia mechi ya Yanga na Etoile du Sahel ya Kombe la Shirikisho ndani ya Uwanja wa Taifa kabla ya kiama kingine cha England.
    Wakitoka tu Taifa kuna vibarua viwili kwenye runinga zao siku hiyo saa 1:30 usiku, Chelsea itakuwa inacheza na Man United katika Ligi Kuu England wakati Arsenal itacheza na Reading katika nusu fainali ya Kombe la FA. Ikaushie hiyo.
    Yanga inayopewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara mzimu huu baada ya kuzizidi nguvu Simba na Azam, itakuwa na kibarua cha kujitengenezea mazingira ya kusonga mbele kwenye raundi ya pili ya Shirikisho dhidi ya timu ngumu ya Etoile ambayo ina bifu na Simba kwa vile haijawalipa mamilioni ya usajili wa Emmanuel Okwi ingawa Fifa imeamuru Mnyama alipwe.
    Unajua Yanga ilichofanya? Baada ya kuzing’oa BDF ya Botswana na Platinum ya Zimbabwe, sasa imeingia na gia mpya kwenye mechi nne zilizobaki kufuzu hatua ya makundi wakianzia na mechi ya Jumamosi.
    Katika mechi hizo nne Yanga imeweka mezani burunguti la Sh288 milioni kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa na inafuta rekodi ya Simba ambayo imekuwa ikiwakejeli kwenye uwanja wa Taifa.
    Simba inawakejeli Yanga kwa mambo mawili; inawaambia Yanga kwamba wamezibahatisha BDF na Platinum na kwamba ndege yao ya mwisho Afrika ni pale watakapoifuata Etoile, lakini pia inawaambia kwamba hawawezi kufikia rekodi yao ya hatua ya makundi mwaka 2003.
    Simba ilifuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa mwaka huo kwa kuitoa Zamalek ya Misri ambao ni Waarabu kama ilivyo Etoile ya Tunisia inayoanza na Yanga Dar es Salaam.
    Lakini Yanga ni kama wameikomesha Simba kwani dau walilotenga kwenye mechi hizo nne ni sawa na mishahara ya kulipa wafanyakazi wote wa Simba kujumuisha wachezaji na makocha kwa miezi minne na chenji inabaki.
    Simba kwa mwezi inatumia Sh60 milioni kulipa mishahara, ambapo fungu linaweza kulipa mishahara ya miezi minne.
    Yanga hutumia Sh85milioni kulipa mshahara kwa mwezi.
    Habari za uhakika ambazo Mwanaspoti inazo ni kwamba Yanga imepitisha bajeti ya kutumia si chini ya dola 40,000 (Sh72 milioni) katika kila mchezo itakayocheza kuanzia sasa kimataifa kuiandaa timu kiufundi pamoja na majukumu mengine ya nje ya uwanja ilimradi kusaka ushindi.
    Mmoja wa vigogo wa Yanga amedokeza kwamba lengo lao ni kuingia kwenye hatua ya makundi na kurejesha hadhi ya Yanga ambayo imekuwa ikiipigania kwa misimu kadhaa ikiwa ni pamoja na kuajiri wataalamu ghali kufikia hatua hiyo.
    Etoile waja na rekodi
    Yanga wanakutana na Etoile du Sahel ambayo haijawahi kushinda chini ya mabao 7-0 inapocheza na timu ya Afrika Mashariki. Desemba mwaka 2006, Etoile ilitwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho ikiwa chini ya kocha wa sasa Faouzi Benzarti kwa kuishinda klabu ya FAR Rabat ya Morocco.
    Lakini kwa mara ya kwanza Etoile ilicheza nchini Tanzania na Afrika Mashariki kwenye raundi ya pili ya 16 bora dhidi ya Moro United ambayo kwa wakati huo ilifahamika zaidi kama Chelsea ya Bongo.
    Etoile iliishinda Moro kwa jumla ya mabao 7-1 ambapo katika mchezo wa kwanza uliopigwa jijini Dar es Salaam Etoile walishinda 4-1, kisha wakaishinda bao 3-0 kwenye mchezo wa marudiano uliochezwa kule Tunisia.
    Kwenye takwimu za mtandao wa CAF zinaonesha kuwa klabu ya Etoile haijawahi kucheza dhidi ya klabu nyingine ya Afrika Mashariki katika miaka ya hivi karibuni zaidi ya Moro ambayo ilishajifia.
    Kocha Mkuu wa Etoile, Faouzi Benzarti ameuambia mtandao mmoja wa michezo wa Tunisia akisema: “Nilishawahi kwenda Tanzania mwaka 2006 na nilifanikiwa kuishinda moja ya timu ya nchi hiyo (Moro United) ambayo kwa wakati huo ilikuwa ikishiriki Shirikisho.
    “Naamini tutakapoenda Tanzania tutapata ushindi na tutakaporudi nyumbani pia tutafanya viz



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Yanga yatumia mil288 kuikomesha Simba Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top